NEW YORK YAMJADILI TENA TEMBO, MJADALA WAONGOZWA NA CHELSEA CLINTON, TANZANIA YASHIRIKI

 Mkurugenzi Mtendaji wa  ABC HOME Paulette Cole akiwakaribisha wanajopo na wageni waalikwa katika majadiliano  kuhusu tembo,  majadiliano hayo yalifanyika siku ya jumanne usiku  Jijini New York.
Chelsea Clinton, Makamu Mwenyekiti wa Clinton Foundation,  na ambaye aliongoza majadiliano hayo  akiwatambulisha wanajopo, kutoka kushoto ni  Bw. John Heminway, Balozi Tuvako Manongi,    kati kati ni Chelsea  Bint wa Rais Bill na Hilary Clinton,  kulia kwa Chelsea ni   Bw. Bryan Christy na  anayefuatia  ni   Bw. Josh Ginsberg kutoka Wildlife Conservation Society. Heminway na Christy ni waandishi na watunga filamu na kwa pamoja wametengeneza filamu ijulikanayo kama  "The Battle for Elephants". Filamu   hiyo  itaonyeshwa  February 27 kupitia  Channel ya National Geograpy.
 Hapana shaka kwamba Hatari ya kutoweka kwa tembo barani afrika,  ni jambo  linalowagusa wengi, washiriki wa majadiliano hayo walitumia fursa hiyo kujifunza siyo tu hatari ya kutoweka kwa  mnyama  huyo, lakini pia uzuri na sifa zake, na namna gani wanaweza kuchangia  kuhakikisha  hatoweki kabisa
 Wadau wa mjadala wakiwa ukumbini
 Waandishi wa habari walikuwepo kwa wingi
Washiriki wakiwa ukumbini

0 comments:

Post a Comment