Rais wa 
Makapera Tanzania, Issa Kwisa Mwaifuge, leo ameamua kuwageuka wafuasi wake rasmi na kuvunja 
katiba ya kundi lake na kuamua kuuaga ukapera rasmi na kumuoa Binti mrembo aliyewahi kushiriki 
shindano kubwa la Miss Tanzania, 2004, Verdiana Kamugisha, ambao kwa pamoja wameamua 
kumeremeta siku ya leo na kufunga ndoa yao katika Kanisa la Lutheran lililopo mitaa ya Sinza jijini 
Dar es Salaam. Na hapa ni wakati wakiwa katika sherehe ya ndoa yao inayoendelea muda huu katika 
Ukumbi wa Msasani Makuni. Picha Zote na www.sufianimafoto.blogspot.com
 Bwana 
Harusi, Issa Kwisa (kushoto) akisebeneka na Suleiman Semunyu, aliyekuwa akipokea zawadi ya keki 
kwa niaba ya ITV.
 Maharusi, 
wakipozi kwa picha na wafanyakazi wa Star Tv, baada ya kuwakabidhi zawadi ya 
keki.
 Hapa 
ilikuwa ni muda wa Kwaito..........
 Sehemu 
ya wageni waalikwa.....
 Wadau 
kutoka (kulia) ni James Range, Joseph Mpangala na Martine Mauya, wakipozi kwa picha mbele ya 
kamera ya Sufiaimafoto.

 Baadhi 
ya wafanyakazi wa ITV ambao ni wafanyakazi wenzake na Bwana Harusi, wakipozi kwa picha, baada 
ya kukabidhiwa zawadi ya keki na Bwana harusi.
 Baadhi 
ya wafanyakazi wa Chanel Ten, wakipozi kwa picha ya pamoja baada ya kupokea zawadi ya 
Keki.
 Sehemu 
ya wageni waalikwa,..
Salum 
Mkambala, akisebeneka kwa staili yake wakati akielekea kupokea zawadi ya keki kwa niaba ya 
wafanyakazi wenzake wa Chanel Ten.









0 comments:
Post a Comment