MAHAFALI YA KWANZA YA KIDATO CHA NNE KWA WAATHIRIKA WA NDOA NA MIMBA ZA UTOTONI SHULE YA AGAPE

Wahitimu 29 wa kidato cha nne shule ya Sekondari Agape Knowledge Open School wakiingia ukumbini wakati wa mahafali ya kwanza katika shule hiyo leo Ijumaa Oktoba 20,2017- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Maandamano kuelekea ukumbini 
Mgeni rasmi na viongozi mbalimbali wakiwa katika maandamano kuelekea ukumbini
Mgeni rasmi ,Afisa Elimu Taaluma mkoa wa Shinyanga,James Malima kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akizungumza wakati wa mahafali ya kwanza ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Agape Knowledge Open School
Afisa Elimu Taaluma mkoa wa Shinyanga,James Malima akizungumza katika mahafali hayo.Kushoto ni mwenyekiti wa mtaa wa Busambilo kata ya Chibe ilipo shule ya  Agape Knowledge Open School, Charles Mayunga. Kulia ni Mkurugenzi wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP),linalomiliki shule hiyo,John Myola.
Wahitimu wa kidato cha nne wakiimba wakati wa mahafali hayo
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akizungumza wakati wa mahafali hayo ambapo aliwataka wazazi kuacha tabia ya kuozesha watoto kwa tamaa ya mali na badala yake wawapeleke shule
Wahitimu wakifurahia jambo wakati Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akizungumza.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akisisitiza "Mtoto wa Kike Shule"
Mwenyekiti wa mtaa wa Busambilo kata ya Chibe ilipo shule ya  Agape Knowledge Open School Charles Mayunga akilishukuru shirika hilo kwa kuwapa elimu watoto ambao wameokolewa katika ndoa
Wanafunzi wanaobaki wanaosoma katika shule ya Agape Knowledge Open School wakiimba wimbo kulishukuru shirika la AGAPE jinsi linavyosaidia watoto wa kike
Mkuu wa shule  ya sekondari Agape Knowledge Open School ,Adili Haruni Nyaluke akielezea historia ya shule hiyo
Wanawake waliopatiwa elimu ya ujasiriamali na shirika la AGAPE wakiimba na kucheza wakati wa mahafali hayo
Wazazi na walezi wakiwa katika mahafali hayo
Wahitimu wa kidato cha nne wakiwa ukumbini
Wahitimu wa kidato cha nne wakiimba na kucheza
Wahitimu wakiimba wakati wa mahafali hayo
Wageni waalikwa wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea wakati wa mahafali hayo
Wazazi na wageni waalikwa wakiwa katika eneo la tukio
Wanafunzi kutoka shule ya Sekondari Tinde wakiwa katika mahafali hayo
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne katika shule hiyo akitoa ushuhuda kuhusu mimba na ndoa za utotoni wakati wa mahafali hayo
Wanafunzi wanaobaki wakicheza muziki
Wahitimu wa kidato cha nne katika shule hiyo wakisoma risala kwa mgeni rasmi
Wanafunzi wanaobaki wakisoma shairi
MC Mwamba akitoa maelekezo wakati wa mahafali hayo
Kaimu afisa elimu msingi wilaya ya Shinyanga Beatrice Mbonea akizungumza wakati wa mahafali hayo
Wageni waalikwa na wafanyakazi wa shirika la AGAPE wakiwa katika eneo la tukio
Mgeni rasmi ,Afisa Elimu Taaluma mkoa wa Shinyanga,James Malima akitoa cheti cha kufanya vizuri katika masomo kwa mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne katika shule ya Agape Knowledge Open School. 
Mhitimu akishikana mkono na mgeni rasmi wakati akipokea cheti
Mhitimu akishikana mkono na mgeni rasmi wakati wa zoezi la ugawaji vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao
Zoezi la utoaji vyeti linaendelea
Zoezi la utoaji vyeti linaendelea
Wageni waalikwa wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea
Mahafali yanaendelea
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akimwongoza mgeni rasmi Afisa Elimu Taaluma mkoa wa Shinyanga,James Malima (kulia) kwenda kuangalia ujenzi wa majengo mbalimbali unaoendelea katika shule hiyo ambayo sasa ina jengo moja tu linaloonekana pichani ambalo linatumika kama darasa lakini pia kama bweni la wanafunzi.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akielezea kuhusu ujenzi huo
Mkurugenzi wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP),John Myola akielezea kuhusu ujenzi wa majengo katika shule hiyo mpya inayokabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile upungufu wa samani,ukosefu wa umeme na maji
Afisa Elimu Taaluma mkoa wa Shinyanga,James Malima akiondoka katika eneo panapojengwa majengo mbalimbali katika shule hiyo.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog