HAPPY BIRTHDAY YA MAMAA WA MITINDO ASIA KHAMSIN IDAROUS YAFANA KWENYE KIOTA CHA NYUMBANI LOUNGE
Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Mamaa wa Mitindo Asia Khamsin Idarous, akizungumza machache kabla ya kukata cake kwenye mnuso wake wa kumbukumbu ya kuzaliwa iliyofanyika kwenye kiota cha Nyumbani Lounge.
Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Mamaa wa Mitindo Asia Khamsin Idarous jana alisheherekea siku yake ya kuzaliwa na ndugu, jamaa na marafiki katika mnuso wa nguvu uliofanyika kwenye kiota cha Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam. Zifuatazo ni picha mbalimbali za matukio katika mnuso huo wa nguvu.(Picha zote na MOblog)
Aunty Asia Idarous akikata ji-cake lake la kutimiza miaka 54 ya kuzaliwa kwake kwenye mnuso wa nguvu uliofanyika Nyumbani Lounge.
Kata Cake tule......asiyeimba hali...Happy Birthday dear Asia.....Happy Birthday to youuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu...!!! We Love Aunty Long Live and Stay Blessed.....Mwaaaaah...!!!
Mkuu wa kaya ya Nyumbani Lounge Captain Gardner G. Habash alipewa heshima ya kuwa mtu wa kwanza kulishwa cake na Birthday Girl Bi. Asia Khamsin Idarous.
Mama mwenye nyumba Lady Jay Dee akishow love na Aunty Asia Khamsin Idarous.
Picha juu na chini ni ndugu, jamaa na marafiki wa Aunty Asia Idarous wakilishwa cake.
Paul Mashauri alikuwa miongoni mwa wadau waliojumuika na Mkongwe wa ubunifu wa mavazi Aunty Asia Khamsin Idarous kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.
Mdau Moddy Bawazir naye aliwakilisha.
Mbunifu wa Mavazi Martin Kadinda a.k.a Mzee wa Single Button naye alikuwepo.
Aunty Asia Khamsin Idarous akiserebuka na wadau ndani ya kiota cha Nyumbani Lounge.
Old is Gold na mimi nimo....Hapana chezea Mamaa wa mitindo.
Mbunifu wa Mavazi Mustafa Hassanali na wadau wengine wakipata Ukodak na Aunty Asia Khamsin Idarous.
Aunty Asia Idarous na Ukodak.
Aunty Asia Idarous akishow love na binti yake ndani ya nyumbani Lounge.
Thank you for coming......love you all....!!
MAMASALMA AMPOKEA MALKIA MAXIMA WA UHOLANZI NA BAADAYE AHUDHURIA DHIFA YA KITAIFA ILIYOANDALIWA NA RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpokea Malkia Maxima wa Uholanzi mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akipokea ua kutoka kwa kijana mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuanza ziara ya siku 3 nchini Tanzania.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi ili kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete tarehe 11.12.2013.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi kwa ajili ya mazungumzo na dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akigonganisha glass/cheers na Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mama Salma wakati wa dhifa ya kitaifa ambayo walimwandalia mgeni huyo huko Ikulu tarehe 11.12.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI
Malkia Maxima wa Uholanzi akipokea ua kutoka kwa kijana mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuanza ziara ya siku 3 nchini Tanzania.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi ili kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete tarehe 11.12.2013.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi kwa ajili ya mazungumzo na dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akigonganisha glass/cheers na Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mama Salma wakati wa dhifa ya kitaifa ambayo walimwandalia mgeni huyo huko Ikulu tarehe 11.12.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI
MAELFU WAFURIKA KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA UHURU WA TANZANIA BARA
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya 
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi alipokua akiwasili 
uwanja wa Uhuru wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru 
leo jijini Dar es salaam.Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Generali Davis 
Mwamunyange.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya 
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akipokea salam ya Rais na kupigiwa mizinga 
21 kutoka kwa gwaride la vikosi vya majeshi ya Ulinzi ya Tanzania leo 
uwanja wa Uhuru mara baada ya kuwasili.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya 
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya majeshi ya 
Ulinzi na usalama leo uwanja wa Uhuru wakati wa maadhimisho ya miaka 52 
ya Uhuru.
Sehemu
 ya askari wa vikosi vya ulinzi na usalama wakiwa wamesimama kwa 
ukakamavu wakati kabla ya kamanda wa gwaride kumkaribisha Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kukagua gwaride hilo
 leo jijini Dar es salaam.
Mke
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma 
Kikwete  akiwasili jukwaa kuu la Uwanja wa Uhuru wakati wa sherehe za 
maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo.
 Gwaride likipita mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kwa mwendo wa haraka.
Rais
 Jakaya Kikwete na Amiri Jeshi Mkuu akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi
 Generali Davis Mwamunyange wakati gwaride la vikosi vya Ulinzi na 
Usalama likipita mbele ya jukwaa kuu  la uwanja wa Uhuru kwa mwendo wa 
haraka.
Baadhi
 ya Maofisa wa jeshi wakipiga saluti wakati wimbo wa Taifa ukiimbwa 
wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru leo jijini Dar es salaam.
Wananchi
 wa mkoa wa Dar es salaam waliojitokeza kuhudhuria maadhimisho ya miaka 
52 ya Uhuru uwanja wa Uhuru leo jijini Dar es salaam.
Vijana
 wa halaiki kutoka Tanzania Bara na Visiwani wakitamka kauli mbiu ya 
maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo jijini Dar es 
salaam ambayo ni “ Vijana ni Nguzo ya Rasilimali Watu,Tuwaamini, 
Tuwawezeshe na Tuwatumie kwa Manufaa ta Taifa Letu”
Vijana
 wa halaiki wakiendelea kuwasilisha jumbe mbalimbali kama inavyoonekana 
mfano wa mnyama aina ya simba kuashiria utalii katika hifadhi  za 
wanyama za Tanzania.
Vijana wa halaiki wakionyesha ukakamavu.
Ujumbe ukiwasilishwa kwa njia ya picha kuhusu viongozi wapigania Uhuru wa Tanzania Bara, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya 
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akitoa hatuba fupi kwa watanzania wakati wa
 maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara, Hatuba yake licha ya
 kujaa maneno ya kumkumbuka rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini  Mzee 
Nelson Rolihlahla Mandela Madiba  aliyeaga dunia juzi nchini Afrika ya 
Kusini imesisitiza Upendo, Amani, Mshikamano miongoni mwa  watanzania na
 kukemea tabia ya baadhi ya viongozi kulipiza kisasi pindi waingiapo 
madarakani.
Rais
 wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein (kushoto), Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (katikati) na Mkuu wa Majeshi 
Generali Davis Mwamunyange wakisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa 
na Idara ya Habari (MAELEZO) leo katika uwanja wa Uhuru wakati wa 
Maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru.
Raia
 wa kigeni waliohudhuria sherehe za miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara 
wakisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa na Idara ya Habari 
(MAELEZO) leo.
Rais
 Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi Generali Davis 
Mwamunyange alipokua akisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa na 
Idara ya Habari (MAELEZO) leo.
Mwenyekiti
 wa Chama cha Demokrasia na Maendelo Freeman Mbowe akiwa miongoni mwa 
viongozi wa vyama vya siasa waliohudhuria maadhimisho ya miaka 52 ya 
Uhuru.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO





























