HAPPY BIRTHDAY YA MAMAA WA MITINDO ASIA KHAMSIN IDAROUS YAFANA KWENYE KIOTA CHA NYUMBANI LOUNGE
Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Mamaa wa Mitindo Asia Khamsin Idarous, akizungumza machache kabla ya kukata cake kwenye mnuso wake wa kumbukumbu ya kuzaliwa iliyofanyika kwenye kiota cha Nyumbani Lounge.
Mbunifu Mkongwe wa Mavazi nchini Mamaa wa Mitindo Asia Khamsin Idarous jana alisheherekea siku yake ya kuzaliwa na ndugu, jamaa na marafiki katika mnuso wa nguvu uliofanyika kwenye kiota cha Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam. Zifuatazo ni picha mbalimbali za matukio katika mnuso huo wa nguvu.(Picha zote na MOblog)
Aunty Asia Idarous akikata ji-cake lake la kutimiza miaka 54 ya kuzaliwa kwake kwenye mnuso wa nguvu uliofanyika Nyumbani Lounge.
Kata Cake tule......asiyeimba hali...Happy Birthday dear Asia.....Happy Birthday to youuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu...!!! We Love Aunty Long Live and Stay Blessed.....Mwaaaaah...!!!
Mkuu wa kaya ya Nyumbani Lounge Captain Gardner G. Habash alipewa heshima ya kuwa mtu wa kwanza kulishwa cake na Birthday Girl Bi. Asia Khamsin Idarous.
Mama mwenye nyumba Lady Jay Dee akishow love na Aunty Asia Khamsin Idarous.
Picha juu na chini ni ndugu, jamaa na marafiki wa Aunty Asia Idarous wakilishwa cake.
Paul Mashauri alikuwa miongoni mwa wadau waliojumuika na Mkongwe wa ubunifu wa mavazi Aunty Asia Khamsin Idarous kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.
Mdau Moddy Bawazir naye aliwakilisha.
Mbunifu wa Mavazi Martin Kadinda a.k.a Mzee wa Single Button naye alikuwepo.
Aunty Asia Khamsin Idarous akiserebuka na wadau ndani ya kiota cha Nyumbani Lounge.
Old is Gold na mimi nimo....Hapana chezea Mamaa wa mitindo.
Mbunifu wa Mavazi Mustafa Hassanali na wadau wengine wakipata Ukodak na Aunty Asia Khamsin Idarous.
Aunty Asia Idarous na Ukodak.
Aunty Asia Idarous akishow love na binti yake ndani ya nyumbani Lounge.
Thank you for coming......love you all....!!
MAMASALMA AMPOKEA MALKIA MAXIMA WA UHOLANZI NA BAADAYE AHUDHURIA DHIFA YA KITAIFA ILIYOANDALIWA NA RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpokea Malkia Maxima wa Uholanzi mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akipokea ua kutoka kwa kijana mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuanza ziara ya siku 3 nchini Tanzania.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi ili kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete tarehe 11.12.2013.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi kwa ajili ya mazungumzo na dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akigonganisha glass/cheers na Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mama Salma wakati wa dhifa ya kitaifa ambayo walimwandalia mgeni huyo huko Ikulu tarehe 11.12.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI
Malkia Maxima wa Uholanzi akipokea ua kutoka kwa kijana mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuanza ziara ya siku 3 nchini Tanzania.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima akiongozana na mwenyeji wake Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakiangalia ngoma mbalimbali za utamaduni zilizokuwa zikicheza wakati wa mapokezi ya mgeni huyo Uwanja wa ndege tarehe 11.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi ili kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na Rais Dkt. Jakaya Kikwete tarehe 11.12.2013.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu, Malkia Maxima wa Uholanzi kwa ajili ya mazungumzo na dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni huyo tarehe 11.12.2013.
Malkia Maxima wa Uholanzi akigonganisha glass/cheers na Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mama Salma wakati wa dhifa ya kitaifa ambayo walimwandalia mgeni huyo huko Ikulu tarehe 11.12.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI
MAELFU WAFURIKA KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA UHURU WA TANZANIA BARA
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi alipokua akiwasili
uwanja wa Uhuru wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru
leo jijini Dar es salaam.Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Generali Davis
Mwamunyange.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akipokea salam ya Rais na kupigiwa mizinga
21 kutoka kwa gwaride la vikosi vya majeshi ya Ulinzi ya Tanzania leo
uwanja wa Uhuru mara baada ya kuwasili.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya majeshi ya
Ulinzi na usalama leo uwanja wa Uhuru wakati wa maadhimisho ya miaka 52
ya Uhuru.Sehemu
ya askari wa vikosi vya ulinzi na usalama wakiwa wamesimama kwa
ukakamavu wakati kabla ya kamanda wa gwaride kumkaribisha Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kukagua gwaride hilo
leo jijini Dar es salaam.Mke
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma
Kikwete akiwasili jukwaa kuu la Uwanja wa Uhuru wakati wa sherehe za
maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo. Gwaride likipita mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kwa mwendo wa haraka.Rais
Jakaya Kikwete na Amiri Jeshi Mkuu akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi
Generali Davis Mwamunyange wakati gwaride la vikosi vya Ulinzi na
Usalama likipita mbele ya jukwaa kuu la uwanja wa Uhuru kwa mwendo wa
haraka.Baadhi
ya Maofisa wa jeshi wakipiga saluti wakati wimbo wa Taifa ukiimbwa
wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru leo jijini Dar es salaam.
Wananchi
wa mkoa wa Dar es salaam waliojitokeza kuhudhuria maadhimisho ya miaka
52 ya Uhuru uwanja wa Uhuru leo jijini Dar es salaam.Vijana
wa halaiki kutoka Tanzania Bara na Visiwani wakitamka kauli mbiu ya
maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo jijini Dar es
salaam ambayo ni “ Vijana ni Nguzo ya Rasilimali Watu,Tuwaamini,
Tuwawezeshe na Tuwatumie kwa Manufaa ta Taifa Letu”Vijana
wa halaiki wakiendelea kuwasilisha jumbe mbalimbali kama inavyoonekana
mfano wa mnyama aina ya simba kuashiria utalii katika hifadhi za
wanyama za Tanzania.
Vijana wa halaiki wakionyesha ukakamavu.Ujumbe ukiwasilishwa kwa njia ya picha kuhusu viongozi wapigania Uhuru wa Tanzania Bara, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akitoa hatuba fupi kwa watanzania wakati wa
maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara, Hatuba yake licha ya
kujaa maneno ya kumkumbuka rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini Mzee
Nelson Rolihlahla Mandela Madiba aliyeaga dunia juzi nchini Afrika ya
Kusini imesisitiza Upendo, Amani, Mshikamano miongoni mwa watanzania na
kukemea tabia ya baadhi ya viongozi kulipiza kisasi pindi waingiapo
madarakani.Rais
wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein (kushoto), Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (katikati) na Mkuu wa Majeshi
Generali Davis Mwamunyange wakisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa
na Idara ya Habari (MAELEZO) leo katika uwanja wa Uhuru wakati wa
Maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru.Raia
wa kigeni waliohudhuria sherehe za miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania Bara
wakisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa na Idara ya Habari
(MAELEZO) leo.Rais
Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi Generali Davis
Mwamunyange alipokua akisoma Jarida la Nchi Yetu linalochapishwa na
Idara ya Habari (MAELEZO) leo.Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendelo Freeman Mbowe akiwa miongoni mwa
viongozi wa vyama vya siasa waliohudhuria maadhimisho ya miaka 52 ya
Uhuru.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO